Matatizo katika matumizi
Mara nyingi kondomu inashindwa kazi na kuruhusu maambukizi kwa sababu:
1. Ina vitundu vidogovidogo kama aina zote za mpira. Ukubwa wa vitundu hivyo ukipimwa: ni mikron 5, wakati ukubwa wa virusi ya Ukimwi (HIV) ni mikron 0.1 tu, yaani kila kitundu ni kikubwa mara 50 kuliko virusi.
2. Wakati wa kuitumia kuna nguvu ya msukumo au mkandamizo, mpishano wa ngozi zake mbili, msuguano wa mpira kati ya watu wawili. Matokeo ni kondomu kuchunika na hatimaye kulika kwa sababu dawa ya kuihifadhi inachanganyikana na tindikali za uke.
3. Pengine kondomu wakati wa ngono hutoka au kupasuka.
Pamoja na hayo:
4. Ingebidi kufuata kanuni kumi za namna sahihi ya kutumia kondomu. Hii inamhangaisha mwanamume kuifikiria sana wakati wa ngono, ikizuia umoja wake na mwenzake na kupunguza raha ya wote wawili. Kutofikia msisimko kunamtesa sana mwanamke moyoni.
5. Wanawake wengine badala ya furaha wanapatwa na maumivu kwa sababu ya msuguano kati ya kondomu na ukuta laini wa uke. Matokeo yake ni ukuta huo kutokwa daima na aina ya majimaji.
Mtazamo wa maadili
Kondomu nyingi baada ya kutumika zunatupwa popote, hata barabarani kama hii. Pengine watoto wanaziokota na kuzitumia kama vipulizo.
Wapo wanaopinga matumizi ya kondomu hata kwa hoja za maadili kama ifuatavyo.
Lengo la kuzuia vijidudu visilete maradhi na hatimaye kifo ni zuri; vilevile pengine familia inahitaji kupanga uzazi.
Hata hivyo lengo jema halihalalishi njia mbaya mbele ya Mungu.
Ni muhimu kuchagua njia ya kufaa pande zote, na kuchunguza ukweli wa maneno ya wanaohimiza kutumia kondomu.
Kondomu inavuruga utaratibu, maana, thamani na heshima ya ndoa ikiingilia kiini chake kwa kuzuia umoja wa miili ya mume na mke: badala ya tendo la ndoa kuna watu wawili wanaosugua mpira kwa viungo vya uzazi; uwezekano wa kuzaa mtoto unapungua sana.
Dhambi hiyo ni kubwa zaidi ikifanywa nje ya ndoa: kwa vyovyote inawatenganisha wote wawili na Mungu badala ya kuwaunganisha naye katika kuendeleza uumbaji.
Uhamasishaji wa matumizi ya kondomu unaua dhamiri za watu waone ubaya katika maradhi na mimba wasione uovu wa dhambi wala matokeo yake ya kiroho, hasa ikitumika nje ya ndoa au kabla ya ndoa.
Kwa mtazamo huo, mtetezi na msambazaji wa kondomu anatenda hasa dhambi za: 1. kudanganya kibiashara (kutapeli kwamba ni kinga imara, wakati si hivyo); 2. kumsaidia jirani kuzini au walau kuzuia vibaya uzazi katika ndoa; 3. kusababisha kifo cha watu wengi watakaoambukizwa hata baada ya miaka kutokana na baadhi ya kondomu kufeli.
Wengine wanalaumu kondomu, hasa za plastiki, kwa kuchafua mazingira.
Friday, 7 December 2018
Madhara ya kope za bandia
Haya Hapa Madhara ya Kuweka Kope za Bandia Kwenye Macho..
Mapokeo ya urembo wa kisasa katika nchi zinazoendelea ni sehemu ya mchango wa urembo na mvuto tunaouona kwa baadhi ya wasichana na wanawake ambao kwa hakika unaleta hamasa ya kuangalia.
Hata hivyo, urembo huu huja na hatari zake ambazo wengi wanaweza kuzichukulia poa kwa kuwa hazitokei kwa haraka ama katika muda unaoweza kutolewa ushahidi kwa sasa.
Moja kati ya urembo unaofanywa na wanawake wengi wa kisasa ni kuweka kope za bandia juu ya kope halisi, kweli wengi wanakuwa na mvuto wa aina yake wakikuangalia hasa mtoto wa kiume. Lakini hatari inayotokana na urembo huo ni kubwa zaidi ya matokeo ya muda mfupi.
Wataalam wanaeleza kuwa kope za bandia ambazo hugundishwa kwa kutumia gundi ya nywele inayotumika kugundisha nywele bandia kwa wenye vipara inaweza kuwa chanzo cha upofu wa mtumiaji.
Gundi hiyo hupukutika taratibu sana kiasi cha kutoshtukiwa na kuelekea kwenye mboni ya jicho ambayo ndio moyo wa ‘kuona’. Endapo mtumiaji ataendelea kwa muda mrefu kutumia kope hizi bandia anaweza kujikuta anakuwa na tatizo la kuona ama hata upofu wa haraka katika maisha yake ya baadae.
Hata hivyo, hatari kubwa imeelekezwa kwa maduka ama vibanda vinatumia vifaa vya bei nafuu ikiwemo gundi inayotumika. Ukwepaji wa gharama ama kutokuwa na uwezo wa kutumia gharama kubwa kunamuingiza mrembo kwenye hatari zaidi.
Kuwa mwangalifu, urembo usiwe chanzo cha kuhatarisha afya yako. Kumbuka Afya ni uhai wa mwili wako.rajabsimba338@gmail.com
Mapokeo ya urembo wa kisasa katika nchi zinazoendelea ni sehemu ya mchango wa urembo na mvuto tunaouona kwa baadhi ya wasichana na wanawake ambao kwa hakika unaleta hamasa ya kuangalia.
Hata hivyo, urembo huu huja na hatari zake ambazo wengi wanaweza kuzichukulia poa kwa kuwa hazitokei kwa haraka ama katika muda unaoweza kutolewa ushahidi kwa sasa.
Moja kati ya urembo unaofanywa na wanawake wengi wa kisasa ni kuweka kope za bandia juu ya kope halisi, kweli wengi wanakuwa na mvuto wa aina yake wakikuangalia hasa mtoto wa kiume. Lakini hatari inayotokana na urembo huo ni kubwa zaidi ya matokeo ya muda mfupi.
Wataalam wanaeleza kuwa kope za bandia ambazo hugundishwa kwa kutumia gundi ya nywele inayotumika kugundisha nywele bandia kwa wenye vipara inaweza kuwa chanzo cha upofu wa mtumiaji.
Gundi hiyo hupukutika taratibu sana kiasi cha kutoshtukiwa na kuelekea kwenye mboni ya jicho ambayo ndio moyo wa ‘kuona’. Endapo mtumiaji ataendelea kwa muda mrefu kutumia kope hizi bandia anaweza kujikuta anakuwa na tatizo la kuona ama hata upofu wa haraka katika maisha yake ya baadae.
Hata hivyo, hatari kubwa imeelekezwa kwa maduka ama vibanda vinatumia vifaa vya bei nafuu ikiwemo gundi inayotumika. Ukwepaji wa gharama ama kutokuwa na uwezo wa kutumia gharama kubwa kunamuingiza mrembo kwenye hatari zaidi.
Kuwa mwangalifu, urembo usiwe chanzo cha kuhatarisha afya yako. Kumbuka Afya ni uhai wa mwili wako.rajabsimba338@gmail.com
Subscribe to:
Comments (Atom)
Kazi na Mchango wa Dkt. Johannes L. Lukumay katika kupigania maendeleo ya jamii
Dkt. Johannes L. Lukumay Mgombea Ubunge - Arumeru Magharibi Dkt. Johannes Lembulung’ Lukumay alianza taaluma yake ya afya zaidi ya miaka ...
-
The Best 8 Free and Open Source Library Management Software Solutions For many of us, nothing seems more important than reading a book. “W...
-
VIDONDA VYA TUMBO Ugonjwa wa vidonda vya tumbo hutokea iwapo kidonda cha ukubwa wa angalau wa nusu sentimita kitatokea kwenye sehemu yeyot...