VIJUE VYAKULA VINAVYOSAIDIA KUONGEZA KINGA YA MWILI
Watu wengi tumekuwa tukijali kazi zetu za kila siku bila kujali hali ya afya zetu matokeo yake kumekuwa na ongezeko kubwa la vifo vya ghafla. Suala la kula pengine ndilo nguzo ya kwanza ya afya ya binadamu Mwili ukiwa sawia bila shaka utaweza kufanya mambo yako yote, na usipokuwa sawa basi hutaweza kutimiza lengo lako lolote!
Hivi ni yakula kadhaa vinavyoweza kukusaidia kuongeza kinga ya Mwili wako
*Yogurt (yogati)*
Hutengenezwa kwa kutumia maziwa ya ng’ombe na kimea, hupatikana kwa ladha mbalimbali kulingana na matakwa yako, yogati pengine ndio chakula kinachoongoza kwa kuogeza Kinga ya mwili wako
*PARACHICHI*:
Ukilinganisha na matunda mengine, tunda hili lina virutubisho vingi zaidi na hutakiwi kulikosa kwenye mlo wako kila siku kwani lina virutubisho vifuatavyo: Vitamini K ambayo inaweza kuchangia asilimia 36 ya mahitaji yako mwilini, asilimia 30 ya mahitaji yako ya siku ya vitamini B.
Muhimu zaidi ni kwamba parachichi ni moja ya matunda machache ambayo yana kiasi kikubwa cha mafuta mazuri (god fats) hivyo kupunguza hatari ya kuugua magonjwa ya moyo na uzito mkubwa.
*Vitunguu saumu*:
Hupatikana Kila soko Tanzania! Japokuwa vitunguu saumu vimekuwa vikitumika sana kwa ajili ya matibabu ya magonjwa mbalimbali toka enzi za mababu, wataalamu wameshauri pia vitunguu hivi ni chanzo muhimu kwa kinga ya binadamu. Vitumie kwa kutafuna (kama unaweza) au weka kwenye chakula!
*Uyoga*:
Usishangae! Ndio.. hiki ni moja ya vyakula muhimu zaidi kuimarisha afya yako kwani huchangia kiasi kikubwa kuimarisha seli nyeupe za damu zinazofanya kazi ya kupambana na magonjwa mbalimbali!
*Supu ya kuku*
Wengi watahisi ni gharama lakini si kubwa kuzidi gharama ya kumuona daktari! Unywaji wa supu ya kuku ya moto husaidia kuzuia kupungua kwa seli nyeupe za damu vilevile hupunguza uwezekano wa kupata matatizo yanayohusiana na mapafu na mfumo wa hewa kiujumla!
*Viazi vitamu(mbatata)*
Unaweza kuhisi ngozi sio sehemu ya muhimu katika kinga ya binadamu lakini ukweli ni kwamba ngozi ni sehemu ya muhimu sana kwa mwili wa binadamu. Kwa kinga kamili ya mwili wa binadamu tunahitaji Vitamin A ambayo hupatikana kwa wingi kwenye viazi vitamu.
*Karoti*
Karoti zina ziada kubwa ya vitamin pengine kuliko tunda lolote lile hivyo jitahidi kujumuisha karoti kama kiungo kwenye chakula au unaweza kuitafuna ikiwa mbichi!
*Samaki*
Husaidia seli nyeupe kuzalisha ctokins zinatohusika kuzuia baadhi ya magonjwa yanayosababishwa na virusi hasa yale yanayohusiana na mfumo wa hewa nk.
*Matikiti*
Wengi Hudharau lakini tunda hili ni muhimu sana katika afya ya kila siku ya binadamu kwani husaidia kuongeza kiasi cha maji mwilin, madini chuma na kuimarisha seli nyeupe za damu
*TANGO*
Ni moja ya tunda na mboga inayozalishwa kwa wingi zaidi duniani. Kuweza kutumia tango unaweza kukatakata na ukachanganya kwenye kachumbari yako, ama unaweza kutengeneza juisi kwa kutumia blenda yako ukiwa nyumbani.
Asilimia 90 ya tango ni maji ambapo vifuatavyo ni virutubisho vinavyopatikana: Vitamini K kwa ajili ya kuzuia maambukizi, Vitamini C kwa ajili ya kupambana na maambukizi, vitamini B ambayo huzalisha nguvu kwenye mwili na madini ya manganese kwa ajili ya kuimarisha mifupa.
Kwenye tango kuna madini ya potassium na magnesium kwa ajili ya afya ya moyo pia lina kemikali inayoitwa lignans ambayo hupatikana pia kwenye kabeji na vitunguu ambayo kazi ya lignans ni kupunguza hatari ya kuugua magonjwa ya moyo, pia muungano wa lignin na bakteria wazuri walioko kwenye mfumo wa usagaji chakula husaidia kupunguza hatari ya kuugua badhi ya saratani kama saratani ya matiti, kizazi, na saratani ya tezi dume.
*Maji*
Kama kuna Kitu cha kwanza kwa uhai wa binadamu basi ni maji. Bila kunywa maji ya kutosha bado utakuwa katika hatari ya kupata magonjwa mbalimbali. Angalau lita moja na nusu hadi lita tatu kwa siku ni muhimu kwa afya yako!.
NB: TUMIA CHAKULA KAMA DAWA NA USITUMIE DAWA KAMA CHAKULA
Usisahau ku comment na ku share
Monday, 28 October 2019
Thursday, 17 October 2019
VIDONDA VYA TUMBO
Ugonjwa wa vidonda vya tumbo hutokea iwapo kidonda cha ukubwa wa angalau wa nusu sentimita kitatokea kwenye sehemu yeyote ya ukuta wa tumbo au utumbo wa binadamu.
Kwa kawaida tatizo hili huleta maumivu makali sana ya tumbo ingawa si lazima kila maumivu ayapatayo mgonjwa husababishwa na vidonda vya tumbo.
Chanzo, dalili, tiba na Madhara ya ugonjwa wa vionda vya tumbo (PUD)
Yafaham yote hayo hapa👇👇👇
https://schoolpvh.blogspot.com/p/vidonda.html?m=1
Ugonjwa wa vidonda vya tumbo hutokea iwapo kidonda cha ukubwa wa angalau wa nusu sentimita kitatokea kwenye sehemu yeyote ya ukuta wa tumbo au utumbo wa binadamu.
Kwa kawaida tatizo hili huleta maumivu makali sana ya tumbo ingawa si lazima kila maumivu ayapatayo mgonjwa husababishwa na vidonda vya tumbo.
Chanzo, dalili, tiba na Madhara ya ugonjwa wa vionda vya tumbo (PUD)
Yafaham yote hayo hapa👇👇👇
https://schoolpvh.blogspot.com/p/vidonda.html?m=1
Saratani ya Tezi Dume - Chanzo na Tiba
Tatizo jingine linaloathiri tezi dume ni saratani ya tezi dume. Saratani ya tezi dume inashika nafasi ya tatu kwa kusababisha vifo vinavyotokana na saratani kwa wanaume wa umri mbalimbali duniani. Aidha ni chanzo kikuu cha vifo vinavyosababishwa na saratani kwa wanaume wa umri miaka 70 na kuendelea. Hata hivyo, ni nadra sana kwa saratani hii kuwapata wanaume chini ya miaka 40.
Soma zaidi hapa👇👇👇
https://RAJAB SIMBA .blogspot.com/p/saratani.html?m=1
Tatizo jingine linaloathiri tezi dume ni saratani ya tezi dume. Saratani ya tezi dume inashika nafasi ya tatu kwa kusababisha vifo vinavyotokana na saratani kwa wanaume wa umri mbalimbali duniani. Aidha ni chanzo kikuu cha vifo vinavyosababishwa na saratani kwa wanaume wa umri miaka 70 na kuendelea. Hata hivyo, ni nadra sana kwa saratani hii kuwapata wanaume chini ya miaka 40.
Soma zaidi hapa👇👇👇
https://RAJAB SIMBA .blogspot.com/p/saratani.html?m=1
Wednesday, 19 June 2019
Friday, 7 December 2018
MATATIZO YA MATUMIZI YA KONDOM
Matatizo katika matumizi
Mara nyingi kondomu inashindwa kazi na kuruhusu maambukizi kwa sababu:
1. Ina vitundu vidogovidogo kama aina zote za mpira. Ukubwa wa vitundu hivyo ukipimwa: ni mikron 5, wakati ukubwa wa virusi ya Ukimwi (HIV) ni mikron 0.1 tu, yaani kila kitundu ni kikubwa mara 50 kuliko virusi.
2. Wakati wa kuitumia kuna nguvu ya msukumo au mkandamizo, mpishano wa ngozi zake mbili, msuguano wa mpira kati ya watu wawili. Matokeo ni kondomu kuchunika na hatimaye kulika kwa sababu dawa ya kuihifadhi inachanganyikana na tindikali za uke.
3. Pengine kondomu wakati wa ngono hutoka au kupasuka.
Pamoja na hayo:
4. Ingebidi kufuata kanuni kumi za namna sahihi ya kutumia kondomu. Hii inamhangaisha mwanamume kuifikiria sana wakati wa ngono, ikizuia umoja wake na mwenzake na kupunguza raha ya wote wawili. Kutofikia msisimko kunamtesa sana mwanamke moyoni.
5. Wanawake wengine badala ya furaha wanapatwa na maumivu kwa sababu ya msuguano kati ya kondomu na ukuta laini wa uke. Matokeo yake ni ukuta huo kutokwa daima na aina ya majimaji.
Mtazamo wa maadili
Kondomu nyingi baada ya kutumika zunatupwa popote, hata barabarani kama hii. Pengine watoto wanaziokota na kuzitumia kama vipulizo.
Wapo wanaopinga matumizi ya kondomu hata kwa hoja za maadili kama ifuatavyo.
Lengo la kuzuia vijidudu visilete maradhi na hatimaye kifo ni zuri; vilevile pengine familia inahitaji kupanga uzazi.
Hata hivyo lengo jema halihalalishi njia mbaya mbele ya Mungu.
Ni muhimu kuchagua njia ya kufaa pande zote, na kuchunguza ukweli wa maneno ya wanaohimiza kutumia kondomu.
Kondomu inavuruga utaratibu, maana, thamani na heshima ya ndoa ikiingilia kiini chake kwa kuzuia umoja wa miili ya mume na mke: badala ya tendo la ndoa kuna watu wawili wanaosugua mpira kwa viungo vya uzazi; uwezekano wa kuzaa mtoto unapungua sana.
Dhambi hiyo ni kubwa zaidi ikifanywa nje ya ndoa: kwa vyovyote inawatenganisha wote wawili na Mungu badala ya kuwaunganisha naye katika kuendeleza uumbaji.
Uhamasishaji wa matumizi ya kondomu unaua dhamiri za watu waone ubaya katika maradhi na mimba wasione uovu wa dhambi wala matokeo yake ya kiroho, hasa ikitumika nje ya ndoa au kabla ya ndoa.
Kwa mtazamo huo, mtetezi na msambazaji wa kondomu anatenda hasa dhambi za: 1. kudanganya kibiashara (kutapeli kwamba ni kinga imara, wakati si hivyo); 2. kumsaidia jirani kuzini au walau kuzuia vibaya uzazi katika ndoa; 3. kusababisha kifo cha watu wengi watakaoambukizwa hata baada ya miaka kutokana na baadhi ya kondomu kufeli.
Wengine wanalaumu kondomu, hasa za plastiki, kwa kuchafua mazingira.
Mara nyingi kondomu inashindwa kazi na kuruhusu maambukizi kwa sababu:
1. Ina vitundu vidogovidogo kama aina zote za mpira. Ukubwa wa vitundu hivyo ukipimwa: ni mikron 5, wakati ukubwa wa virusi ya Ukimwi (HIV) ni mikron 0.1 tu, yaani kila kitundu ni kikubwa mara 50 kuliko virusi.
2. Wakati wa kuitumia kuna nguvu ya msukumo au mkandamizo, mpishano wa ngozi zake mbili, msuguano wa mpira kati ya watu wawili. Matokeo ni kondomu kuchunika na hatimaye kulika kwa sababu dawa ya kuihifadhi inachanganyikana na tindikali za uke.
3. Pengine kondomu wakati wa ngono hutoka au kupasuka.
Pamoja na hayo:
4. Ingebidi kufuata kanuni kumi za namna sahihi ya kutumia kondomu. Hii inamhangaisha mwanamume kuifikiria sana wakati wa ngono, ikizuia umoja wake na mwenzake na kupunguza raha ya wote wawili. Kutofikia msisimko kunamtesa sana mwanamke moyoni.
5. Wanawake wengine badala ya furaha wanapatwa na maumivu kwa sababu ya msuguano kati ya kondomu na ukuta laini wa uke. Matokeo yake ni ukuta huo kutokwa daima na aina ya majimaji.
Mtazamo wa maadili
Kondomu nyingi baada ya kutumika zunatupwa popote, hata barabarani kama hii. Pengine watoto wanaziokota na kuzitumia kama vipulizo.
Wapo wanaopinga matumizi ya kondomu hata kwa hoja za maadili kama ifuatavyo.
Lengo la kuzuia vijidudu visilete maradhi na hatimaye kifo ni zuri; vilevile pengine familia inahitaji kupanga uzazi.
Hata hivyo lengo jema halihalalishi njia mbaya mbele ya Mungu.
Ni muhimu kuchagua njia ya kufaa pande zote, na kuchunguza ukweli wa maneno ya wanaohimiza kutumia kondomu.
Kondomu inavuruga utaratibu, maana, thamani na heshima ya ndoa ikiingilia kiini chake kwa kuzuia umoja wa miili ya mume na mke: badala ya tendo la ndoa kuna watu wawili wanaosugua mpira kwa viungo vya uzazi; uwezekano wa kuzaa mtoto unapungua sana.
Dhambi hiyo ni kubwa zaidi ikifanywa nje ya ndoa: kwa vyovyote inawatenganisha wote wawili na Mungu badala ya kuwaunganisha naye katika kuendeleza uumbaji.
Uhamasishaji wa matumizi ya kondomu unaua dhamiri za watu waone ubaya katika maradhi na mimba wasione uovu wa dhambi wala matokeo yake ya kiroho, hasa ikitumika nje ya ndoa au kabla ya ndoa.
Kwa mtazamo huo, mtetezi na msambazaji wa kondomu anatenda hasa dhambi za: 1. kudanganya kibiashara (kutapeli kwamba ni kinga imara, wakati si hivyo); 2. kumsaidia jirani kuzini au walau kuzuia vibaya uzazi katika ndoa; 3. kusababisha kifo cha watu wengi watakaoambukizwa hata baada ya miaka kutokana na baadhi ya kondomu kufeli.
Wengine wanalaumu kondomu, hasa za plastiki, kwa kuchafua mazingira.
Madhara ya kope za bandia
Haya Hapa Madhara ya Kuweka Kope za Bandia Kwenye Macho..
Mapokeo ya urembo wa kisasa katika nchi zinazoendelea ni sehemu ya mchango wa urembo na mvuto tunaouona kwa baadhi ya wasichana na wanawake ambao kwa hakika unaleta hamasa ya kuangalia.
Hata hivyo, urembo huu huja na hatari zake ambazo wengi wanaweza kuzichukulia poa kwa kuwa hazitokei kwa haraka ama katika muda unaoweza kutolewa ushahidi kwa sasa.
Moja kati ya urembo unaofanywa na wanawake wengi wa kisasa ni kuweka kope za bandia juu ya kope halisi, kweli wengi wanakuwa na mvuto wa aina yake wakikuangalia hasa mtoto wa kiume. Lakini hatari inayotokana na urembo huo ni kubwa zaidi ya matokeo ya muda mfupi.
Wataalam wanaeleza kuwa kope za bandia ambazo hugundishwa kwa kutumia gundi ya nywele inayotumika kugundisha nywele bandia kwa wenye vipara inaweza kuwa chanzo cha upofu wa mtumiaji.
Gundi hiyo hupukutika taratibu sana kiasi cha kutoshtukiwa na kuelekea kwenye mboni ya jicho ambayo ndio moyo wa ‘kuona’. Endapo mtumiaji ataendelea kwa muda mrefu kutumia kope hizi bandia anaweza kujikuta anakuwa na tatizo la kuona ama hata upofu wa haraka katika maisha yake ya baadae.
Hata hivyo, hatari kubwa imeelekezwa kwa maduka ama vibanda vinatumia vifaa vya bei nafuu ikiwemo gundi inayotumika. Ukwepaji wa gharama ama kutokuwa na uwezo wa kutumia gharama kubwa kunamuingiza mrembo kwenye hatari zaidi.
Kuwa mwangalifu, urembo usiwe chanzo cha kuhatarisha afya yako. Kumbuka Afya ni uhai wa mwili wako.rajabsimba338@gmail.com
Mapokeo ya urembo wa kisasa katika nchi zinazoendelea ni sehemu ya mchango wa urembo na mvuto tunaouona kwa baadhi ya wasichana na wanawake ambao kwa hakika unaleta hamasa ya kuangalia.
Hata hivyo, urembo huu huja na hatari zake ambazo wengi wanaweza kuzichukulia poa kwa kuwa hazitokei kwa haraka ama katika muda unaoweza kutolewa ushahidi kwa sasa.
Moja kati ya urembo unaofanywa na wanawake wengi wa kisasa ni kuweka kope za bandia juu ya kope halisi, kweli wengi wanakuwa na mvuto wa aina yake wakikuangalia hasa mtoto wa kiume. Lakini hatari inayotokana na urembo huo ni kubwa zaidi ya matokeo ya muda mfupi.
Wataalam wanaeleza kuwa kope za bandia ambazo hugundishwa kwa kutumia gundi ya nywele inayotumika kugundisha nywele bandia kwa wenye vipara inaweza kuwa chanzo cha upofu wa mtumiaji.
Gundi hiyo hupukutika taratibu sana kiasi cha kutoshtukiwa na kuelekea kwenye mboni ya jicho ambayo ndio moyo wa ‘kuona’. Endapo mtumiaji ataendelea kwa muda mrefu kutumia kope hizi bandia anaweza kujikuta anakuwa na tatizo la kuona ama hata upofu wa haraka katika maisha yake ya baadae.
Hata hivyo, hatari kubwa imeelekezwa kwa maduka ama vibanda vinatumia vifaa vya bei nafuu ikiwemo gundi inayotumika. Ukwepaji wa gharama ama kutokuwa na uwezo wa kutumia gharama kubwa kunamuingiza mrembo kwenye hatari zaidi.
Kuwa mwangalifu, urembo usiwe chanzo cha kuhatarisha afya yako. Kumbuka Afya ni uhai wa mwili wako.rajabsimba338@gmail.com
Subscribe to:
Comments (Atom)
Kazi na Mchango wa Dkt. Johannes L. Lukumay katika kupigania maendeleo ya jamii
Dkt. Johannes L. Lukumay Mgombea Ubunge - Arumeru Magharibi Dkt. Johannes Lembulung’ Lukumay alianza taaluma yake ya afya zaidi ya miaka ...
-
The Best 8 Free and Open Source Library Management Software Solutions For many of us, nothing seems more important than reading a book. “W...
-
VIDONDA VYA TUMBO Ugonjwa wa vidonda vya tumbo hutokea iwapo kidonda cha ukubwa wa angalau wa nusu sentimita kitatokea kwenye sehemu yeyot...